Tuesday, November 1, 2011

Mkutano ukiendelea





Wafanyakazi wa TCMP na washirika wao wakiwa katika  kazi ya kuandaa mpango wa utekelezaji wa mradi wa Pwani kwa mwaka 2012 katika hoteli ya Livingstone, Bagamoyo. Mkutano wa siku mbili unamalizika kesho tarehe 2/11/2011. Kabla ya kuanza kwa mkutano asubuhi, kiongozi toka Baraza la Usimamizi wa Mazingira la Taifa (NEMC) Bw. Muheto anayeonekana katikati katika picha ya kwanza alitoa hotuba ya ufunguzi rasmi. Picha ya pili na ya tatu ni washiriki wakifuatilia ufunguzi huo. Picha ya nne ni mwakilishi wa mradi kutoka Kituo cha Rasilimali za Pwani (CRC) cha Chuo Kikuu cha Rhode Island Elin Torell akiweka kumbukumbu ya baadhi ya masuala yaliyojadiliwa.

No comments:

Post a Comment