Tuesday, October 9, 2012

Kijijini Mwembeni, Pangani Jana

 Wanakijiji wa Mwembeni Baada ya Kukutana na wafanyakazi wa Mradi wa Pwani pamoja na waandishi wa habari na maofisa wa wilayani ya Pangani jana. Ziara hiyo ilikuwa ikifuatilia utekelezaji wa shughuli za mradi kijijini humo
 Wanakijiji wakielezea wageni wao jinsi kilimo cha mazao yaliyozoeleka kama mpunga, minazi na mahindi yalivyoathirika na mabadiliko ya tabia nchi na hivyo kuamua kuanza majaribio ya kilimo cha migomba


Mashina ya migomba inayostahimili ukame yakionekana yakianza kuchipua katika shamba la majaribio ya jinsi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi katika kijiji cha Mwembeni. Mashamba haya yameanzishwa na wananchi kwa kupata msaada wa ushauri na mbegu kutoka Mradi wa Pwani. Pia kupata msaada wa kitaalam kutoka halmashauri ya wilaya ya Pangani.

Takwimu za mashirika ya kimataifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa asilimia kubwa ya watu duniani wataanza kutegemea zaidi ndizi kama zao kuu la chakula kutokana na uwezekano wa mazao mengi ya chakula kushindwa kuhimili mabadiliko ya tabia nchi.