Friday, August 17, 2012

Kuwavua Tembo Kola


Kikosi cha angani kikijiandaa kupaa

Kikosi cha angani kikijiandaa kutua porini

                                        Kikosi cha ardhini kikielekea maeneo ya tukio

Kikosi cha ardhini kikikaribia eneo la tukio

Dk. Alfred Kikoti wa Kituo cha Utafiti wa Tembo Duniani akifanya kazi ya kuvua kola


Kazi ya kumvua tembo kola ikiendelea

Dk. Kikoti na mwenzake wakiangalia jeraha la risasi ambalo tembo aliyevuliwa kola alikuwa nalo. Hii inaonyesha kuendelea kwa vitendo vya ujangili dhidi ya nyara za taifa

Kazi imekamilika

Mradi wa Kufuatilia Mwenendo wa Tembo katika Mbuga ya Taifa ya Saadani na Pori la Hifadhi la Wambi Mbiki ulianza mwaka 2010 kwa kuwavisha tembo 17 kola ili kuweza kuwafuatilia kwa njia ya satelaiti. Baada ya kukusanya taarifa za kutosha, hivi majuzi kazi ya kuwavua kola hizo ilifanyika katika Pori la Hifadhi la Wami Mbiki kama picha zinavyoonyesha hapo juu. Mradi huo ni sehemu ya miradi iliyoko chini ya Mradi wa TCMP-Pwani unaofadhiliwa na Shirika la Misaada ya Kimataifa la Watu wa Marekani (USAID).
(Picha zote kwa hisani ya Dk. Alfred Kikoti wa Kituo cha Tembo Duniani)