Wadau Wetu

Suala la msingi kwa  TCMP ni kufanya kazi na mashirika ambayo yatatusaidia kuleta pamoja utaalam tofauti na rasilimali ili kufanikisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazoikabili pwani yetu. Washirikka wetu ni pamoja na ngazi zote za serikali ya  Tanzania ikiwa ni pamoja na wizara mbalimbali katika ngazi ya kitaifa, serikali za mitaa, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali,  miradi na programu nyingine zinazotekelezwa nchini, mashirika ya kiraia, wanajamii, sekta binafsi na vyuo vikuu. Mkusanyiko huu wa washirika ikiwa ni pamoja na watu mmoja mmoja na mashirika na taasisi unaruhusu TCMP kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokabili jamii za pwani na hatimaye kuleta mabadiliko katika ngazi na maeneo mbalimbali ya kijiografia.

  




Copywright@TCMP 2011