Wednesday, July 4, 2012

Angalia Pwani Yetu


Kilimo bora cha mpunga katika shamba la majaribio kwenye kijiji cha Kitonga, Bagamoyo ambalo linapata msaada kutoka Mradi wa TCMP-Pwani


Kilimo duni cha mpunga katika kijiji cha Sange, Pangani


Kilimo duni cha ufuta katika kijiji cha Sange, Pangani


Migomba yenye uwezo wa kustahimili ukame kwenye kijiji cha Mwembeni, Pangani. Kilimo cha aina hii ya migomba kinaweza kuwa njia nzuri ya kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi katika kilimo cha mazao ya chakula kwenye Pwani Yetu


Njia ya kuingia kwenye msitu wa asili wa Mziha, ambao unahifadhiliwa kwa imani za jadi kuheshimu "Mzimu wa Mziha" katika kijiji cha Mwembeni, Pangani. Maarifa ya jadi kama haya yanaweza kuhifadhi vizuri mazingira ya Pwani Yetu.




Muonekano bora katika maingilio ya Mto Msangazi katika kijiji cha Sange na Mto Pangani katika kijiji cha Msaraza wilayani Pangani. Maeneo haya yanahitaji kutunzwa ili kuhakikisha mazingira endelevu ya Pwani Yetu


Uhaba wa maji ni miongoni mwa changamoto nyingi zinazoikabili Pwani Yetu. Hali hiyo inazidi kujidhihirisha zaidi katika kipindi hiki ambacho mabadiliko ya tabia nchi yamepiga hodi kwenye vijiji vingi vya Pwani. Picha zikionyesha uhaba wa maji katika kijiji cha Mwembeni, wilayani Pangani.
Upandaji wa mimea aina ya Ipomea ni njia bora ya kuzuia mmomomyoko wa udongo ambao unasababishwa na kuongezeka kwa ukubwa na nguvu za mawimbi ya bahari katika Pwani Yetu. Hali hii inasemekana kuzidishwa zaidi na mabadiliko ya tabia nchi. Picha inaonyesha maandalizi  ya upandaji wa mimea hiyo katika ufukwe wa kijiji cha Sange.

Picha zote na Don Obadue wa Coastal Resources Center (CRC)