Monday, November 12, 2012

Ujasiriamali Unaopunguza Matumizi ya Kuni




Rukia Seif wa kijiji cha Mkalamo akijishughulisha na kazi ya uokaji mikate katika jiko banifu. Picha ya chini ni Mkurugenzi wa Mradi wa Pwani, Baraka Kalangahe akiangalia jiko hilo katika ziara yake ya hivi karibuni ya kukagua shughuli zinazofanywa na wanavikundi wanaopata msaada kutoka Mradi wa Pwani katika wilaya ya Pangani. Jiko hilo banifu hutumia kuni chache, halitoi moshi mwingi na pia linamfanya Rukia kujishughulisha na shughuli ambazo ni rafiki kwa mazingira. 

Angalia Ujasiriamali na Uzazi wa Mpango



 
Mradi wa TCMP-Pwani unahamasisha matumizi ya dhana ya uzazi wa mpango na ujasiriamali katika kutunza mazingira. Pciha ya kwanza ikimuonyesha kijana akiwa amevaa fulana inayohamasisha uzazi wa mpango. Picha za chini zinaonyesha wanakijiji wa Sakura-Kwakiubuyu wilaya Pangani wakiwa katika biashara zao ndogondogo ambazo zinawafanya kuondokana na shughuli za uharibifu wa mazingira. Wajasiriamali hawa wamepata mikopo kutoka Chama cha Kuweka na Kukopa (SACCOS) cha Songambele.