Wednesday, March 7, 2012

Mabadiliko ya Tabia Nchi ni Halisi

                                                                                         
"
Angalia jinsi mawimbi yalivyomomonyoa ukingo wa Bahari. Ukuta huu unaosemekana kujengwa miaka ya 80 katika eneo la Jambiani, huko Unguja, sasa umebaki kifusi                             

                              Hiki ni choo, ambacho kimechukukuliwa na mmomonyoko unaotokana na mawimbi makubwa ya bahari 

                                         
 Washiriki wa mkutano wa Kamati ya Kusimamia Miradi inayofadhiliwa na Watu wa Marekani ulioandaliwa na Mradi wa TCMP-Pwani wakishuhudia athari za mabadiliko ya tabia nchi kandokando mwa Bahari ya Hindi katika eneo la Jambiani, huko Unguja

Majani haya katika mwambao wa Paje, Zanzibar, yanasemekana kuwa na uwezo mkubwa wa kupunguza athari za mawimbi ya bahari yanayotokana na mabadiliko ya tabia nchi

Mabadiliko ya tabia nchi katika ukanda wa pwani ikiwa ni pamoja na Zanzibar sasa ni halisi. Jamii zinaozishi karibu na bahari maeneo ya Bagamoyo, Pangani na Zanzibar zimeanza kushuhudia kuongezeka kwa nguvu ya mawimbi ya bahari na hivyo kuathiri makazi na shughuli zao za kiuchumi. Picha zinaonyesha mmomonyoko wa kingo za bahari unaosemekana kutokana na mabadiliko ya tabia nchi katika eneo la Jambiani, Zanzibar. Pia zinaonyesha washiriki wa Mkutano wa Kamati ya Kusimamia Miradi inayofadhiliwa na Watu wa Marekani ulioandaliwa na TCMP-Pwani

No comments:

Post a Comment