Monday, April 8, 2013

Ziara ya Mshauri wa Kiufundi wa Masuala ya Idadi ya Watu, Afya na Mazingira wa USAID Matthew Erdman

Mjadala na vikundi vya SACCOS na Waelimishaji Rika Mkange
 
UZIKWASA ni mshirika mkuu wa TCMP Pwani wilayani Pangani
 
Kubadilishana uzoefu na taarifa na mkurugenzi wa UZIKWASA
 
Kugawa vifaa vya elimu na mawasiliano kwa Wasambazaji wa Vifaa na Huduma za PHE katika jamii (CBDs)
 
Picha ya pamoja na wadau wa Mkange
 
Picha ya pamoja na wadau wa Sakura
 
 
 
 
 
 

Friday, March 8, 2013

Kilimo cha Mabadiliko ya Tabia Nchi


Moja ya kazi za kitengo cha mabadiliko ya tabia nchi katika mradi wa TCMP Pwani ni kuhamasisha wananchi kupanda mazao yanayostahimili ukame, magonjwa na yanayokomaa haraka. Kazi hii inafanyika kwa kushirikiana na taasisi za utafiti wa kilimo nchini, wataalam wa kilimo wa wilaya, kata na katika ngazi ya kijiji. Mashamba ya ufuta bora yanaonekana katika kijiji cha Sange, Pangani.
 

Ofisa anayeshughulika na mabadiliko ya tabia nchi katika mradi wa TCMP Pwani, Bw Wilbard Mkama (kushoto) akitembelea mashamba ya majaribio ya kilimo bora cha ufuta katika kijiji cha Sange. Kulia ni bwana shamba wa kijiji hicho. 
 

 
 Migomba nayo ni zao ambalo limeonekana kuhimili ukame katika kijiji cha Mwembeni, Pangani.
 

Thursday, March 7, 2013

Mafunzo ya PHE

Mafunzo ya Idadi ya Watu, Afya na Mazingira (PHE) yaliyofanyika mjini Bagamoyo kuanzia tarehe 18 hadi 28 Februari yalikusanya wataalam wa mazingira kutoka nchi mbalimbali duniani. Mafunzo hayo yalikuwa ya vitendo zaidi. Juu kikundi cha kujadiliana kikiwa katika majdala mkali
 
Mafunzo yaliyokuwa ya vitendo zaidi yalitumia  dhana mbalimbali za kufundishia zilitumika
 
Michezo ya kuigiza pia ilitumika ili kufikisha ujumbe kwa washiriki katika mafunzo hayo
 



Friday, February 15, 2013

Watoaji Huduma za Uzazi wa Mpango Katika Jamii

Watoaji Huduma za Uzazi wa Mpango (CBDs) katika jamii wana mchango mkubwa wa kupeleka huduma za afya na uzazi wa mpango karibu zaidi na jamii wanamoishi. Mmoja wa watoaji huduma hizo akiwa dukani kwake ambalo pia hutumika kama duka la kuuza kondomu katika kijiji cha Kwakibuyu/Sakura wilayani Pangani.

Monday, November 12, 2012

Ujasiriamali Unaopunguza Matumizi ya Kuni




Rukia Seif wa kijiji cha Mkalamo akijishughulisha na kazi ya uokaji mikate katika jiko banifu. Picha ya chini ni Mkurugenzi wa Mradi wa Pwani, Baraka Kalangahe akiangalia jiko hilo katika ziara yake ya hivi karibuni ya kukagua shughuli zinazofanywa na wanavikundi wanaopata msaada kutoka Mradi wa Pwani katika wilaya ya Pangani. Jiko hilo banifu hutumia kuni chache, halitoi moshi mwingi na pia linamfanya Rukia kujishughulisha na shughuli ambazo ni rafiki kwa mazingira. 

Angalia Ujasiriamali na Uzazi wa Mpango



 
Mradi wa TCMP-Pwani unahamasisha matumizi ya dhana ya uzazi wa mpango na ujasiriamali katika kutunza mazingira. Pciha ya kwanza ikimuonyesha kijana akiwa amevaa fulana inayohamasisha uzazi wa mpango. Picha za chini zinaonyesha wanakijiji wa Sakura-Kwakiubuyu wilaya Pangani wakiwa katika biashara zao ndogondogo ambazo zinawafanya kuondokana na shughuli za uharibifu wa mazingira. Wajasiriamali hawa wamepata mikopo kutoka Chama cha Kuweka na Kukopa (SACCOS) cha Songambele. 

Tuesday, October 9, 2012

Kijijini Mwembeni, Pangani Jana

 Wanakijiji wa Mwembeni Baada ya Kukutana na wafanyakazi wa Mradi wa Pwani pamoja na waandishi wa habari na maofisa wa wilayani ya Pangani jana. Ziara hiyo ilikuwa ikifuatilia utekelezaji wa shughuli za mradi kijijini humo
 Wanakijiji wakielezea wageni wao jinsi kilimo cha mazao yaliyozoeleka kama mpunga, minazi na mahindi yalivyoathirika na mabadiliko ya tabia nchi na hivyo kuamua kuanza majaribio ya kilimo cha migomba


Mashina ya migomba inayostahimili ukame yakionekana yakianza kuchipua katika shamba la majaribio ya jinsi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi katika kijiji cha Mwembeni. Mashamba haya yameanzishwa na wananchi kwa kupata msaada wa ushauri na mbegu kutoka Mradi wa Pwani. Pia kupata msaada wa kitaalam kutoka halmashauri ya wilaya ya Pangani.

Takwimu za mashirika ya kimataifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa asilimia kubwa ya watu duniani wataanza kutegemea zaidi ndizi kama zao kuu la chakula kutokana na uwezekano wa mazao mengi ya chakula kushindwa kuhimili mabadiliko ya tabia nchi.