Tuesday, December 20, 2011

Samaki Hawa ni Urithi wa Pwani Yetu


Samaki aina ya Papa akiwa amevuliwa na wavuvi wa kijiji cha Ushongo wilayani Pagani, Tanga


Hawa nao wanachekelea kitoweo aina ya Pweza huko huko Ushongo, Pangani

Thursday, November 24, 2011

Ufugaji wa nyuki


Kuunga mkono au kuanzisha miradi mbadala ya kuwaingizia kipato wakazi wa maeneo ya mwambao wa pwani ni moja ya mfumo unaotumiwa na mradi wa TCMP Pwani ili kuifanya Pwani Yetu kuwa endelevu kwa kupunguza utegemezi wa kupindukia katika rasilimali za bahari.

Wednesday, November 9, 2011

Je wajua?


Mikoko ni moja ya rasilimali muhimu sana katika kuhifadhi mazingira ya pwani na bahari. Huzuia mmomonyoko unaosababishwa na mawimbi ya bahari na pia kutumika kama mazalia ya samaki. Angalia mikoko hii inavyopendeza.


Friday, November 4, 2011

Mkutano Umekwisha




Mkutano wa siku mbili ulihitimishwa na mazungumzo ya kuagana, kila mtu kubeba kilichokuwa cha kwake na picha ya pamoja tarehe 2/11/2011


Tuesday, November 1, 2011

Mkutano ukiendelea





Wafanyakazi wa TCMP na washirika wao wakiwa katika  kazi ya kuandaa mpango wa utekelezaji wa mradi wa Pwani kwa mwaka 2012 katika hoteli ya Livingstone, Bagamoyo. Mkutano wa siku mbili unamalizika kesho tarehe 2/11/2011. Kabla ya kuanza kwa mkutano asubuhi, kiongozi toka Baraza la Usimamizi wa Mazingira la Taifa (NEMC) Bw. Muheto anayeonekana katikati katika picha ya kwanza alitoa hotuba ya ufunguzi rasmi. Picha ya pili na ya tatu ni washiriki wakifuatilia ufunguzi huo. Picha ya nne ni mwakilishi wa mradi kutoka Kituo cha Rasilimali za Pwani (CRC) cha Chuo Kikuu cha Rhode Island Elin Torell akiweka kumbukumbu ya baadhi ya masuala yaliyojadiliwa.

Baada ya kazi kucheza



Wafanyakazi wa TCMP na washirika wao wakisakata rumba baada ya kazi ngumu ya siku nzima ya kuandaa mpango wa utekelezaji wa mradi wa Pwani kwa mwaka 2012 katika hoteli ya Livingstone, Bagamoyo. mkutano wa siku mbili unamalizika kesho tarehe 2/11/2011

Monday, October 31, 2011

Kazi Studioni


Kazi ikiendelea katika Studio ya Redio Pangani FM inayomilikiwa na shirika la Uzima kwa Sanaa (UZIKWASA). Shirika hili ni miongoni mwa Washirika wakuu wa Ushirika wa Kusimamia Mazingira na Rasilimali za Pwani na Bahari ambao hurusha baadhi ya vipindi vyake vya mazingira katika redio hiyo