Kuunga mkono au kuanzisha miradi mbadala ya kuwaingizia kipato wakazi wa maeneo ya mwambao wa pwani ni moja ya mfumo unaotumiwa na mradi wa TCMP Pwani ili kuifanya Pwani Yetu kuwa endelevu kwa kupunguza utegemezi wa kupindukia katika rasilimali za bahari.
Mikoko ni moja ya rasilimali muhimu sana katika kuhifadhi mazingira ya pwani na bahari. Huzuia mmomonyoko unaosababishwa na mawimbi ya bahari na pia kutumika kama mazalia ya samaki. Angalia mikoko hii inavyopendeza.
Wafanyakazi wa TCMP na washirika wao wakiwa katika kazi ya kuandaa mpango wa utekelezaji wa mradi wa Pwani kwa mwaka 2012 katika hoteli ya Livingstone, Bagamoyo. Mkutano wa siku mbili unamalizika kesho tarehe 2/11/2011. Kabla ya kuanza kwa mkutano asubuhi, kiongozi toka Baraza la Usimamizi wa Mazingira la Taifa (NEMC) Bw. Muheto anayeonekana katikati katika picha ya kwanza alitoa hotuba ya ufunguzi rasmi. Picha ya pili na ya tatu ni washiriki wakifuatilia ufunguzi huo. Picha ya nne ni mwakilishi wa mradi kutoka Kituo cha Rasilimali za Pwani (CRC) cha Chuo Kikuu cha Rhode Island Elin Torell akiweka kumbukumbu ya baadhi ya masuala yaliyojadiliwa.
Wafanyakazi wa TCMP na washirika wao wakisakata rumba baada ya kazi ngumu ya siku nzima ya kuandaa mpango wa utekelezaji wa mradi wa Pwani kwa mwaka 2012 katika hoteli ya Livingstone, Bagamoyo. mkutano wa siku mbili unamalizika kesho tarehe 2/11/2011
Kazi ikiendelea katika Studio ya Redio Pangani FM inayomilikiwa na shirika la Uzima kwa Sanaa (UZIKWASA). Shirika hili ni miongoni mwa Washirika wakuu wa Ushirika wa Kusimamia Mazingira na Rasilimali za Pwani na Bahari ambao hurusha baadhi ya vipindi vyake vya mazingira katika redio hiyo